IFAHAMU ASILI YA WAPARE..
Tanzania ni nchi yenye
makabila zaidi ya 120 lakini katika makala hii endelevu nitaanza kwa kuchambua
kabila la wapare, je wapare ni kina nani?
Asili yao ni nini? Wanaishi wapi? Wanajishughulisha na nini? Lakini pia
ni zipi mila na desturi zao?
Ndugu msomaji ungana na
mwandishi wako Ramadhani Gidion katika
kuifwatilia makala hii endelevu itakayokuchambulia mila na desturi za
makabila mbalimbali ndani ya Tanzania pamoja na kutambua vivutio vya asili
vinavyopatikana katika mazingira yao.
Kabila la wapare
linapatikana mkoani Kilimanjaro kaskazini mwa Tanzania katika wilaya ya Same na
Mwanga japo wapo wapare waishio maeneo ya Moshi kama vile
chekereni,himo,uchira, mabungo na moshi mjini, vilevile wanaishi wilayani Hai
kwenye maeneo kama Rundugai na mto weruweru.Mkoani Tanga wapare wanaishi zaidi
lushoto katika maeneo ya Bumbuli na Mavumo.
Asili ya wapare
inasemekana ni Taveta nchini Kenya ambako waliishi huko zaidi ya karne moja na
nusu iliyopita wakijulikana kwa jina la “waasu” kabla ya kuingia Tanganyika
kupitia mpaka wa Taveta.Historia inaeleza kuwa wapare wa mwanzo walifikia
katika miteremko ya mlima kilmanjaro wakiongozwa na machifu wao mashuhuri kama
vile mfumwa (chief) Boazi Mashambo ambako
waligombana na wenyeji ambao ni wachaga na kuhamia milima ya Same na Mwanga
ambayo saivi inafahamika kama milima ya upare.
Wapare wamegawanyika katika makundi mawili wapo wapare wa kaskazini (vampare va mpare ya ughu) hawa huishi wilayani Mwanga kwenye meneo ya ugweno ambao huongea lugha ijulikanayo kama “kigweno” na wapo wanaishi maeneo ya Usangi hawa hutumia lugha ya kipare. Kundi la pili ni wapare wa kusini (vampare va mpare ya kusea) hawa huishi wilayani Same huzungumza kipare jopo kinatofutiana matamshi (lafudhi) na wapare wa usangi.
Kabila hili hujihusisha
zaidi na kilimo cha mahindi,maharagwe, mpunga, na vitunguu hasa kwenye mabonde
maarufu yaliyojaliwa maji na rutuba kama vile bonde la Ruvu,kisiwani, maore na
Ndungu wilayani Same vilevile maeneo ya Ugweno na Usangi wilayani Mwanga ambapo
kilimo cha migomba kimeshamiri zaidi.Same milimani pia kwenye maeneo ya Mbaga
na Gonja kilimo cha migomba na nafaka kama maharagwe na mahindi hutegemewa
zaidi kama zao la chakula katika maisha ya kila siku.Katika eneo la mamba
miamba na Kanza husifika zaidi kwa kilimo cha tangawizi pia yapo mabwawa na
madimbwi mbalimbli yatumikayo katika shughuli za uvuvi kama vile bwawa la
nyumba ya mungu, bwawa la ndungu na dimbwi la msangeni.
Mbali na uwepo wa aridhi nzuri yenye rutuba kwa kilimo katika milima na mabonde ya upare pia vipo vivutio vya utalii wa asili katika maeneo hayo ikiwemo mito maarufu kama vile Hingilili,Rika,Nakombo, Mhoke vuta, Yongoma, Mwetanano pamoja na maporomoko yanayosemekana kuwa marefu kuliko ya ziwa Victoria (Victoria falls) maarufu kama “Ndurumo” yapatikanayo eneo la Gonja Bombo.
Mbali na uwepo wa aridhi nzuri yenye rutuba kwa kilimo katika milima na mabonde ya upare pia vipo vivutio vya utalii wa asili katika maeneo hayo ikiwemo mito maarufu kama vile Hingilili,Rika,Nakombo, Mhoke vuta, Yongoma, Mwetanano pamoja na maporomoko yanayosemekana kuwa marefu kuliko ya ziwa Victoria (Victoria falls) maarufu kama “Ndurumo” yapatikanayo eneo la Gonja Bombo.
Hali kadhalika upareni
kuna hifadhi kubwa ya Taifa ya Mkomazi,Bwawa la Kalimawe na Nyumba ya
mungu,milima ya Kindoroko,mokanda na
Masheko vudee ndolwa.Pia kuna majabali makubwa yavutiayo wataalii kuja kutizama
kama lile la Malameni linalopatikana Mbaga Manka ambalo zamani
inasemekana zilikua zikisikika sauti za wasichana watatu ndani ya jiwe hilo
vilevile kuna jabali la Mhewe linalopatikana vudee ndolwa.
Usikose mwendelezo wa makala hii……
No comments
+255716829257