Habari mpya

MFAHAMU SITI BINTI SAAD MALAIKA WA PWANI YA AFRIKA MASHARIKI..



 
Siti binti Saad ni nani?
Kwa wanao ifahamu  vizuri historia ya pwani ya Afrika mashariki, Siti binti Saad ni mwanamke maarufu sana huko visiwani Zanzibar, alizaliwa mwaka 1880 katika kijiji cha Fumba visiwani humo, baba yake alikuwa mnyamwezi kutoka Tabora na mama yake alikuwa mzigua kutoka Tanga.Alikulia katika familia ya hali duni sana, baba na mama yake walijishughulisha na shughuli za kilimo na ufinyanzi.
Alipatiwa jina la “siti” na waarabu lenye maana ya “mtumwa” kwakua alizaliwa katika kipindi cha biashara ya utumwa katika pwani ya Afrika mashariki katika miaka ya mwanzo ya karne ya 20.
Siti alijaliwa kipaji cha kuimba na sauti tamu ya kumtoa nyoka pangoni aliyoitumia vyema kuzinadi bidhaa zilizofinyangwa na mama yake ili kujikimu na hali ngumu ya maisha katika kipindi hicho cha utumwa wa waarabu visiwani Zanzibar.
 Siti alijipatia umaarufu zaidi baada ya kuhamia mjini kutafuta maisha ambako alijihusisha na uimbaji wa nyimbo za taarabu zenye ujumbe mzito ikiwemo kupigania uhuru ili kikomesha  biashara ya utumwa katika pwani ya Afrika mashariki.
                                         “..siti binti saadi kawa mtu lini,
                                             Kaja na kaniki duni
                                             Kama si sauti angekula nini..”
Ushujaa na uzalendo wa  Siti uliwasisimua wengi wakiwemo waandishi mashuhuru wa vitabu waliotumia kazi zao kuelezea umaarufu wa mwanamke huyu shujaa wa Afrika.Shabani Robert katika kitabu chake “WASIFU WA SITI BINTI SAAD” alitumia ufundi wa hali ya juu kufafanua jinsi Siti alivyokua shujaa mwenye kipaji na utashi mkubwa.
 

No comments

+255716829257