Habari mpya

Nape Nauye apata ajali ya gari

Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Moses Nnauye amepata ajali ya gari leo asubuhi katika Kijiji cha Kibutuka akiwa njiani kuelekea Liwale kwa ajili ya kushiriki kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Lindi.
Pamoja na Nape alikuwa ameambatana na watu wengine wanne ambao wote ni wazima na hamna aliyedhurika.
Mbunge huyo pia alikuwa aungane katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally anayefanya ziara katika Wilaya ya Liwale.

No comments

+255716829257