Habari mpya

SHERIA YA WAENDESHA BAISKELI KATIKA MAKUTANO YA BARABARA.

Image result for SHERIA YA WAENDESHA BAISKELI KATIKA MAKUTANO YA BARABARA.
Na Ramadhani Gidion.
Punguza mwendo na kuwa makini zaidi kwenye makutano kwa sababu madereva wanaweza wasikuone. Kamwe usiamini kuwa madereva wanakuona. Iwapo utaona kuwa makutano hayo yana magari mengi na vigumu kupita, simama na ushuke  kisha tembea na baiskeli yako kuvuka barabara, fuata sehemu ambayo watembea kwa miguu wengine wanapita. Angalia magari yanayopinda mbele yako.
Angalia madereva wanaotoka pembeni mwa barabara wanaweza wasikuone. Usiendeshe upande wa magari yanayoashiria au kupunguza mwendo kupinda kushoto  madereva wa magari makubwa na marefu wakati mwingine hushindwa kuona kuwa wamekupita vizuri kabla ya kupinda kushoto.
 Kupinda kulia, Unapopinda kulia, angalia magari yaliyo nyuma yako, onyesha ishara inayofaa, na iwapo ni salama nenda katikati ya barabara. Subiri hadi kunapokuwa na upenyo ambao ni salama barabarani kabla ya kumalizia kupinda.
Mzunguko, Chukua tahadhari kubwa kwenye mzunguko kwani mara nyingi madereva hushindwa kuwaona na kuwaruhusu waendesha baiskeli. Kwa ujumla ni salama kukaribia mzunguko kwa njia iliyo upande wa kushoto na kuendelea kupita kushoto kwenye mzunguko hicho chukua tahadhari kubwa wakati unaendesha kupitia sehemu ya kutokea, na unaweza kuhitaji kuashiria kulia kuwaonyesha madereva kuwa hutoki kwenye mzunguko.
Angalia magari yanayokatisha kwenye njia yako kuondoka au kuingia kwenye mzunguko. Mara zote ni salama kuyaacha magari marefu kupita kwenye mzunguko kabla ya kuendelea. Iwapo huna uhakika unaweza kuendesha kwa usalama kwenye mzunguko, simama na shuka kwenye baiskeli na utembee nayo kwenye njia ya watembea kwa miguu.
Tumia Kanuni za Uvukaji wakati unapita kwenye barabara ya kuingilia. Ishara zinazoongoza makutano. Fuata maelekezo yanayotolewa na ishara ya taa za barabarani. LAZIMA usimame iwapo ishara ya Highway Code-Inside-Swa.indd Sec1:12 ighway Code-Inside-Swa.indd Sec1:12 9/25/08 3:14:42 PM /25/08 3:14:42 PM 13 taa nyekundu au za njano itaonyeshwa.
 Simama kwenye sehemu iliyoandikwa SIMAMA au fuata nafasi yako kwenye mstari wa magari yanayosubiri.

Chanzo:Kanuni za barabara,wizara ya miundombinu 2008,Tanzania.

No comments

+255716829257