Habari mpya

JIFUNZE KUPIKA KABICHI ZA MAYAI..

Image result for JIFUNZE KUPIKA KABICHI ZA MAYAI..
Kabichi ni aina ya mboga za majani ambayo hupikwa kwa  mapishi tofauti. Unaweza kupika kabichi yenyewe bila kuchanganya na chochote pia  unaweza kupika kwa kuchanganya na nyama, mayai au chochote unachoona kinafaa  mboga yako itakuwa nzuri   na kuweza kuliwa na ugali, wali na hata kupikia pilau.
Leo  tutaangalia jinsi ya kupika kabichi iliyochanganywa na mayai, ambapo tunaanza na mahitaji pamoja na  hatua za kufuata katika upikaji wa kabichi iliyochanganywa na mayai.
-MAHITAJI
·         Kabichi moja ya ukubwa wa wastani
·         Mayai manne (4)
·         Mafuta robo lita
·         Vitunguu vinne (4)
·         Karoti kubwa moja
·         Pilipili manga kiasi
·         Chumvi kiasi kwa ladha

JINSI YA KUPIKA KABICHI HATUA KWA HATUA
1.       Chukua kabichi ulikatekate kisha ulioshe.
2.      Washa jiko lolote ulilonalo liwe la mkaa, gesi au umeme.
3.      Kisha bandika kabichi ulilolikatakata na kuliosha liache liive kidogo kisha ipua.
4.      Menya nyanya, katakata vitunguu, karoti uviweke tayari kwa mapishi.
5.      Bandika sufuria jikoni na utie mafuta ya kupikia, yakipata moto tia vitunguu ukaange mpaka vibadilike rangi kisha tia nyanya ukaange.
6.      Nyanya zikishaiva tia karoti kaanga kidogo.
7.      Baada ya hapo tia pilpili manga pamoja na kabichi ulilolichemsha.
8.     Vunja mayai uliyoandaa na kisha changanya na kabichi ililoungwa tayari na ukoroge hadi mboga yako ikauke.

Mpaka kufikia hapo mboga yetu ya kabichi iliyochanganywa na mayai itakuwa imeiva na tayari kwa kuliwa kwa chakula ukipendacho iwe ugali, wali hata pilau.

No comments

+255716829257