WAZAZI WAASWA KUACHA KUWAPA MAZIWA YA KOPO NA YA NG`OMBE WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MWAKA MMOJA..
Wazazi na
walezi nchini wametakiwa kuacha kutumia maziwa ya kopo na ya Ng’ombe kwa
watoto ambao hawajafikisha mwaka mmoja ili kuwanusuru katika tatizo la
kuchubuka utumbo.
Ushauri
huo ulitolewa jijini Dar es salaam na kaimu mkurugenzi kitengo cha afya
ya uzazi na mtoto, Dk. Georgina Msemo, katika maadhimisho ya
unyonyeshaji yanaayoendelea.
Dk Msemo
alisema maziwa ya ng’ombe yana Casein ambayo haifai kwa mtoto mwenye
umri wa kuzaliwa hadi mwaka mmoja pia alisema maziwa hayo husababisha
mzio, pumu na kusema kwamba maziwa ya mama ni bora na yanayotoa kinga ya
mwili kwa mtoto katika maisha yake yote.
Dk Msemo amesema ………..>>>‘Maziwa
ya mama ni chakula bora kwa mtoto, kwani licha ya kumpa lishe bora pia
humpatia mtoto majianayoyahitaji kwa ukuaji wake katika miezi sita ya
mwanzo‘
>>>’Maziwa mazito na ya njano ambayo huitwa kolostramu yanayotoka siku chache za mwanzo humkinga mtoto dhidi ya maradhi mengi‘:-Dk Msemo.
No comments
+255716829257