KOMBE LA KIMATAIFA LA KLABU: BARCELONA YAILAZA LEICESTER 4-2, AHMED MUSA ANG`ARA..
Mchezaji ghali zaidi kununuliwa na
Leicester City Ahmed Musa, aliyenunuliwa pauni milioni 16 na kuvunja
rekodi ya klabu hiyo, amewafungia mabao yote mawili katika mechi ambayo
wamefungwa 4-2 na Barcelona katika michuano ya Kombe la Kimataifa la
Klabu.
Munir alifungua ukurasa wa mabao kupitia pasi iliyotoka kwa
Lionel Messi kabla ya nyota huyo wa Argentina muda mfupi baadaye
kumuandalia pasi safi Luis Suarez aliyeongoeza la pili katika mchezo huo
uliochezewa uwanja wa Friends Arena mjini Stockholm, Sweden.Munir aliongeza la tatu, kabla ya Musa kukomboa bao moja.
Musa alifanikiwa kukomboa la pili lakini nguvu mpya wa Barca Rafa Mujica, mwenye umri wa miaka 17 pekee, akaifungua Barcelona la nne dakika za mwisho mwisho.
"Msimu uliopita Leicester walishangaza sana katika soka ya Ulaya, na hii ndiyo sababu inayomfanya kila mtu kuupenda mchezo huu," meneja wa Barcelona Luis Enrique alisema baadaye.
Mshambuliaji Jamie Vardy, aliyeongeza muda wa mkataba wake kwa miaka minne mwezi Juni, na Riyad Mahrez, ambaye amehusishwa na kuhamia Arsenal, wote walianza kwenye kikosi cha Leicester kitakachokabiliana na Manchester United katika mechi ya Ngao ya Jamii uwanjani Wembley siku ya Jumapili.
Upande wa Barca, kando na Messi na Suarez, kulikuwa na nyota wengine kama vile Javier Mascherano na Sergio Busquets.
Leicester wataanza kutetea taji lao la Ligi Kuu ya England dhidi ya Hull City ugenini mnamo tarehe 13 Agosti.
No comments
+255716829257