Habari mpya

SERIKALI YAAZIMIA KUWAKOMBOA VIJANA WAHITIMU KATIKA JANGA LA AJIRA..



NA CHAUYA ADAMU.
Kufuatia uhaba wa ajira nchini, serikali kwa kushirkiana na mashirika binafsi imeazimia kutoa mikopo kwa vijana hasa wanaomaliza vyuo vikuu badala ya kusubiri ajira za mojakwamoja kutoka serikalini.
Alipozungumza na vijana katika semina ya ujasiriamali iliyoandaliwa na jukwaa la jamii ya wajasiriamali Tanzania (TASEF), ofisa maendeleo kutoka wizara ya sera, bunge, kazi ajira na vijana ofisi ya waziri mkuua, Godfrey Chacha, amesema katika mchakato wa kupunguza umasikini nchini, serikali kwa kushirikiana na mashirika binafsi imeamua kutoa ajira kwa vijana ili kutatua tatizo la ajira nchini.
“Vijana wanalia na tatizo la ajira kila siku, serikali imeamua kuchukua jukumu la kuwapa mikopo amabayo itawasaidia kujiajiari wenyewe badala ya kusubiri ajira za mojakwamoja” alisema Chacha.
 Chacha ameongeza kuwa mikopo itatolewa kupitia vikundi ambapo vijana wametakiwa  kubuni mawazo ya aina gani ya biashara watakayoifanya.
Hata hivyo amesema kila kikundi kinatakiwa kuwa na usajili ambapo kitaandika barua ya maombi kwenda kwa afisa mtendaji wa kata kwaajili ya utambulisho ambayo itapelekwa mojakwamoja hadi kwa afisa maendeleo wa wilaya au manispaa.
“Mnatakiwa kutengeneza vikundi vyenye usajili kutoka katika halmashauri au manispaa zenu ambapo mtaandika barua za kuomba mkopo huo mkiambatanisha na aina gani ya biashara mtakayofanya”
“hakikisheni mnakuwa na pendekezo (proposal) pamoja na jina la kikundi katiba ambavyo amabapo baada kupata barua kwa mtendaji kata, mtapeleka kwa afisa maendeleo wa wilaya au manispaa na hapo itafika wizarani” Alisema Chacha.
 Chacha amesema serikali itatoa milioni kumi kwa kila kikundi chenye sifa ambapo itakata riba ya asilimia kumi maada ya muda wa miaka miwili.
Kwa upande mwingine, shirika linalosaidia kutatua changamoto za watoto barani Africa (Reach for Change Africa) limesema linahitaji kupata mawazo chanya kutoka kwa vijana juu ya namna ya kuwasaidia watoto nchini, amabapo kupitia ushindani litatoa Milioni arobaini kwa kila mshindi lengo ikiwa ni kuwasaidia vijana kutatua tatizo la ajira kupitia ujasiriamali.
 Redemtha William ni (program assistance) katika shirika hilo, amesema shirika lao linawasidia vijana wasio na ajira kwa kupokea mawazo yao ambayo yatasaidia kutatua changamoto za watoto katika jamii.
  “Katika kupambana na umasikini tumeungana na serikali kuwapatia vijana mitaji kwaajili ya ujasiriamali amabapo tunahitaji wawe wagunduzi  kwa kuja na mawazo yatakayo saidia kutatua changamotomo za watoto katika jamii”
Hata hivyo washiriki wa semina hiyo wamesema tatizo kubwa kwa vijana si swala la ajira pekee lakini ni namana gani ya kuiendesha ajira hiyo amabapo wameiomba serikali kuandaa mafunzo kwa vijana juu ya ujasiriamali kabla ya kuwapa fedha hizo.
Dickson Edward, mhitimu wa chuo cha ustawi wa jamii, amesema kwa kuwa serikali imeshindwa kuwaajiri vijana, kuna ulazima wa kuandaa mafunzo na kozi maalum za ujasiriamali tangu wakiwa chuoni
“Ni wazi kabisa serikali imeshindwa kuwaajiri wahitimu wote wa vyuo vikuu lakini kuna tatizo lingine la vijana kushindwa kuajirika, nadhani kuna umuhimu wa serikali kuandaa mafunzo maalum kwa vijana juu ya ujasiriamali tangu wakiwa vyuoni” alisema Dickson
Dickson ameongeza kuwa serikali lazima irekebishe mitaala vyuoni na hivyo masomo ya ujasiriamali yapewe kipaumbele ili kuwajenga vijana kuwa wajasiriamali.
Kutokana na mlolongo mrefu wa upatikanaji wa mikopo hiyo, Happiness Njovu mhitimu wa chuo kiuu Tumaini tawi la Dar es salaam amesema serikali ipunguze mlolongo huo kwani ni mrefu na utachukua muda kupatikana kwa mikopo hiyo.
“Fikiria utunge  katiba, ufanye usajiri, uandike barua ya maombi kwa mtendaji, uende kwa afisa maendeleo wa wilaya, aipeleke mkoani ndiyo ifike wizarani, huo mkopo utachukua muda kupatikana na na unaweza usipate kabisa”
“ni bora watengeneze fomu maalum tujaze watupatie mkopo kama wana nia ya dhati kutusaidia” alisema Happiness.




No comments

+255716829257