Habari mpya

ZUMA AKUBALI AFRIKA SIO BARA KUBWA ZAIDI.

ZumaImage copyrightGetty
Image captionAfisi ya Zuma imetoa taarifa wiki tano baada ya Zuma kufanya kosa hilo
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ameomba radhi na kusahihisha tamko lake la awali kwamba Afrika ndilo bara kubwa zaidi duniani.
Bw Zuma alitoa matamshi hayo akihutubia dhifa ya jioni ya wafanyabiashara mjini Sandton nchini humo tarehe 9 Desemba mwezi uliopita.
Aliongeza kuwa Afrika ni kubwa kiasi kwamba mabara hayo mengine yanaweza kutoshea ndani ya Afrika.
Alichekwa sana mtandaoni.
Lakini taarifa iliyopakiwa na afisi yake mtandaoni leo inasema: "Afrika bila shaka ndilo bara la pili kwa ukubwa duniani ukizingatia idadi ya watu, na bara kubwa zaidi duniani ni Asia.”
Kwenye taarifa hiyo, afisi hiyo imeonyesha makadirio ya Umoja wa Mataifa kuhusu idadi ya watu mwaka 2015 yanayoonyesha 60% ya watu duniani huishi Asia (4.4 bilioni) na 16% barani Afrika (1.2 bilioni).
Bara Ulaya linafuata kwa kuwa na 10% ya watu (737 milioni).
“Rais amejutia kosa hili.”

No comments

+255716829257