Habari mpya

MMILIKI WA KLABU YA CHELSEA,ROMAN ABRAMOVICH KUJADILI HATIMA YA MOURINHO.

AbramovichImage copyrightPA
Image captionAbramovich anajulikana kwa kuwafuta makocha ambao wanashindwa kuandikisha matokeo mazuri
Mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich amekutana na bodi ya klabu hiyo kujadili hatima ya meneja wa klabu hiyo Jose Mourinho.
Hii ni baada ya klabu hiyo kuandikisha matokeo mabaya sana msimu huu, matokeo ya karibuni zaidi yakiwa kuchapwa 2-1 na Leicester ligini Jumatatu.
Hiyo ilikuwa mara ya tisa kwa Chelsea kushinda Ligi ya Premia katika mechi 16 na sasa wamo alama moja pekee juu ya eneo la kushushwa daraja.
Haijabainika iwapo Mourinho, 52, bado atakuwa kwenye usukani wakati wa mechi kati ya The Blues na Sunderland Jumamosi uwanjani Stamford Bridge.
Abramovich alitangaza kwamba bado alikuwa akimuunga mkono Mourinho Oktoba lakini matokeo hayajaimarika.
Abramovich na wenzake uongozini Chelsea wamekuwa wakimuunga mkono meneja huyo lakini kuna kizungumkuti cha ni hadi lini watasubiri klabu hiyo iimarike.




Tatizo jingine ni kwamba kwa sasa hakuna meneja msifika ambaye hana kazi na anaweza kuitwa upesi kujaza pengo.

Carlo Ancelotti ambaye hana kazi tayari alikuwa Chelsea awali na akafutwa.
Meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola na Diego Simeone Atletico Madrid bado wana majukumu kwa sasa.
Hili limepelekea uvumi kwamba sasa huenda Chelsea ikarudi tena kwa Guus Hiddink kwa mkataba wa muda.
Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 69 alishikilia usukani kwa muda Chelsea mwaka 2009 na kuongoza klabu hiyo kushinda Kombe la FA.
source: BBC

No comments

+255716829257