Habari mpya

WADAU WA MAZINGIRA WAOMBA KIPAUMBELE KUTOKA KWA SERIKALI.

Na Gidion Ramadhani

Arusha.Wadau mbalimbali wanaojishughulisha na utunzaji wa mazingira jijini Arusha wameelezea changamoto mbalimbali wanazozipata katika shughuli hizo ikiwa ni pamoja na kukosa kipaumbele kutoka katika serikali na jamii kwa ujumla.

Walisema hayo wakati walipokua wakizungumza na gazeti hili lilipotembelea eneo wanapofanyia shughuli zao  lililopo Mianzini, jijini Arusha ambako walitaja baadhi ya shughuli wanazozifanya kuwa ni pamoja na uoteshaji wa bustani za miti na maua ambayo huuzwa kwa watu mbalimbali wakiwepo wageni na wenyeji ambayo kwa namna moja husaidia utunzaji wa mwzingira.

 “Tunatengeneza bustani kubwa za miti na maua ya aina mbalimbali ambayo tunawauzia watu kutoka sehemu mbalimbali wakiwemo wenyeji na wageni ikizingatiwa kuwa Arusha ni jiji la kitalii hivyo wageni wengi kutoka ndani na nje ya nchi huitembelea Arusha na kujionea shughuli tunazofanya na asilimia kubwa kuvutiwa nazo” alisema Bi Maria Emmanuel mmoja wa wadau hao.

Wadau hao walizitaja changamoto mbalimbali wanazokumbana nazokumbana nazo kuwa ni kukosa maeneo maalum ya kufanyia shughuli zao amoja na jamii kutotambua mchango wao katika utunzaji wa mazingira..
 “Tatizo kubwa ni kwamba hatuna maeneo maalum tuliyotengewa na serikali kwa ajili ya kufanyia shughuli zetu,tunajikuta tukifanyia pembezoni mwa barabara ambako mara nyingi tunapata misukosuko mingi kutoka kwa wakala wa ujenzi wa barabara(TAN ROAD) hata hivyo jamii inayotuzunguka pia inashindwa kutambua tunachofanya wakati mwingine bustani zetu huvurugwa na mmianzini.

Wameiomba serikali,mashirika yanayojihusisha na utunzaji wa mazingira pamoja na wanajamii wote wenye mapenzi mema na wenye urafiki na mazingira kuwaunga mkono wadau hao ikiwemo kupatiwa maeneo maalum ya kufanyia shughuli zao pamoja na kutolewa elimu ya kutosha kwa jamii nzima juu ya utunzaji wa mazingira na faida zake kwani mazingira bora ndio chanzo cha hali ya hewa nzuri na upatikanaji wa mvua za kutosha.












No comments

+255716829257