Habari mpya

VYOMBO VYA HABARI ENDELEENI KUHABARISHA NA KUFICHUA MAOVU.

Gidion Ramadhani.

Nimatumaini yangu kuwa sote tumeuanza vyema mwaka 2015,shukrani na utukufu vinastahili kuelekezwa kwa mwenyezi mungu muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo mwenye kuneemesha neema kubwa na ndogo,hakika yeye ndie mwenye mamlaka pekee yakutuweka hai mpaka tumeushudia mwaka mpya.
Naamini sote tumeshudia kazi kubwa iliyofanywa na vyombo vya habari tangu mwaka jana 2014 ikiwa ni pamoja na kuibua,kuelimisha,kuhabarisha,kuburudisha pamoja na kuchambua masuala mbalimbali ya kisiasa,kiuchumi na kijamii ndani na nje ya nchi yetu.

Tumeshuhudia  vyombo vya habari vikisimama kidete kutetea unyanyasaji wa watoto mfano mzuri ni kwa Yule aliyeitwa “mototo wa box” ambapo wasamaria wema wenye uchungu na mapenzi ya dhati kwa watoto wanaonyanyasika walipolisikia hilo kupitia vyombo vya habari walijikuta wakilaani vikali vitendo kama hivyo na pia sheria ikafwata mkondo wake kwa wahusika ili iwe funzo kwa wote wenye kuwatendea vibaya watoto.

Miongoni mwa majanga yaliyotikisa nchi ni pamoja na mlipuko wa ugonjwa hatari wa Dengue ambao ungeweza kusababisha maafa makubwa nchini lakini kupitia kampeni kubwa iliyofanywa na vyombo vya habari ili kuhamasisha na kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi juu ya jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo hatimaye kwa Baraka za mungu ugonjwa ukatoweka.

Sanjari na hayo nchi za Afrika magharibi, Sierra leon,Nigeria,Guinea,Senegal na nchi ya jirani,Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo zilijikuta zikigubikwa na wimbi la ugonjwa hatari wa Ebola ambapo mamilioni ya watu walifariki dunia kutokana na ugonjwa huo lakini vyombo vya habari vya ndani na nje vilipambana nab ado vinapambana kikamilifu kuhakikisha vinasambaza habari katika nchi hizo na kote duniani kuwatahadharisha watu juu ya ugonjwa huo na pia kuhamasisha mashirika mbalimbali ya kibinadamu duniani kutoa misaada mbali mbali kwa waathirika ikiwemo kinga,dawa pamoja madaktari bingwa ili kuutokomeza kabisa ugonjwa wa Ebola.

Hata hivyo vyombo vya habari havikuishia hapo hata katika kinyang`anyiro cha miss Tanzania mwaka 2014,ilikua watanzania wapigwe changa la macho lakini vyombo vya habari vilikua macho na kuweka mambo hadharani juu ya udanganyifu wa Bibie Sitti Mtemvu na hatimaye kuvuliwa taji hilo na kuvishwa mwenye vigezo vinavyokubalika.

Tugusie sakata zito la akaunti ya Escrow ambapo almanusra watanzania wapoteze mabilioni ya fedha ya kodi zao pasipo kujijua,zaidi ya billion 300 ziligundulika kuchukuliwa na watu wachache kwa maslahi yao binafsi ikiwa umati wa watanzania,wakubwa kwa wadogo,wakike na wakiume wakiendelea kutaabika katika mateso ya kukosa huduma muhimu za kijamii kama vile hospitali bora hakuna madaktari wanagoma huku dawa hakuna,maji safi na salama bado ni tatizo sugu wakina mama na watoto vijijini hufwata maji kilometa tatu mpaka tano,elimu bora ni bado tatizo shule hazina madawati,vitabu wala maabara,hakuna nyumba za waalimu na bado wanalipwa mishahara midogo.

Vyombo vya habari vililiona hilo na kulifwatilia kwa ukaribu kule bungeni na kutoa taarifa kwa umma hatimaye wahusika kubainika na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Tukiangazia halihalisi ya mwaka huu  2015 yapo mambo mengi yanayokuja mbele yetu ikiwemo mchakato wa katiba mpya ambapo wananchi hutarajiwa kutoa maoni yao, nina imani kuwa vyombo vya habari vitaonesha ushirikiano wa hali ya juu katika suala hili kama ilivyokua mwaka jana wakati wa kutoa maoni juu ya rasimu ya katiba mpya ambapo wananchi walikua makini sana kusikiliza redio,kutizama runinga,kusoma magazeti pamoja na kuperuzi mitandao mbalimbali ya kijamii ili kujua kinachoendelea juu ya mchakato mzima wa katiba mpya.

Hali kadhalika lipo suala jingine nyeti ndani ya huu mwaka ambalo ni uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na madiwani,ni matumaini yangu kuwa kila mtanzania anayo shauku kubwa yakutaka kujua uchaguzi utakuaje na pia naamini vyombo vyetu vya habari vitakua mstari wa mbele kutuhabarisha kila linalojiri katika tukio hili zima la kidemokrasia kuanzia kipindi cha kampeni mpaka uchaguzi.Tutapata kuziskia hoja na sera mbalimbali za wagombea wetu kupitia vyombo vya habari sanjari na kufichuliwa kwa maovu yote yatakayojitokeza kinyume na sheria na utaratibu wa uchaguzi.

Kwa pamoja tumuombe mungu atuongoze tuweze kupata katiba bora yenye kusimamia haki nausawa kwa watu wote na yenye kuleta chachu ya maendeleo katika taifa hili lililojaliwa kila aina ya utajiri zikiwemo mbuga za wanyama,milima mirefu,mito,bahari na maziwa,misitu mikubwa na ardhi yenye rutuba,migodi mikubwa ya madini adimu duniani,nishati ya gesi pamoja na watu wenye busara,ukarimu na upendo wa hali ya juu pia tumuombe mungu atujalie uchaguzi huru na tulivu wa haki na usawa.Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.



                                Waziri wa Habari Michezo na Utamaduni Fenera Mkangala.















No comments

+255716829257