Habari mpya

JIFUNZE KUPIKA MKATE WA BOGA.


Image result for JIFUNZE KUPIKA MKATE WA BOGA.
Mahitaji
·                                  Vikombe 3 vya boga lililosagwa 
·                                  Mafuta kikombe 1 na nusu
·                                  Vikombe 4 vya sukari nyeupe
·                                  Mayai 6
·                                  Unga vikombe 4 na robo tatu
·                                  Baking powder kijiko 1 na nusu cha chai
·                                  Baking soda kijiko 1 na nusu cha chai
·                                  Chumvi kijiko 1 na nusu cha chai
·                                  Mdalasini kijiko 1 na nusu cha chai
·                                  Nutmeg kijiko 1 na nusu cha chai
·                                  Karafuu kijiko 1 na nusu
Maelekezo
·                           Washa oven kwenye nyuzijoto 350°F (176°C) wakati unaandaa mahitaji.
·                           Paka mafuta chombo utakachotumia kuoka mkate kisha nyunyiza unga juu yake. Paka unga uenee vizuri kuzunguka chombo chote. Unga utakaozidi toa.
·                           Kwenye bakuli kubwa, pasua mayai kisha koroga vizuri. Weka boga, mafuta na sukari. Changanya kwa pamoja vizuri.
·                           Kwenye bakuli tofauti – weka unga, baking soda, baking powder, chumvi, mdalasini, nutmeg na karafuu. Changanya vizuri.
·                           Changanya mchanganyiko wa unga ule wa mayai pamoja. Changanya vizuri hadi uwe na uzito wa wastani.
·                           Weka walnuts, changanya. Weka mchanganyiko kwenye chombo cha kuokea.   Weka kwenye oven, tega muda wa saa 1. Muda ukifika, angalia kama imeiva, kisha tena na ujirambe

No comments

+255716829257