Uchambuzi wa album bora za zamani za bongo flava..

Zamani kidogo mwishoni
mwa miaka ya 90 mpaka 2009 hivi ungekuwa sio mwanamuziki uliyekamilika kama
hukuwa na album sokoni! Ili uwe mmoja kati ya wasanii wakali ni lazima Album
yako iliyosheeni ngoma zako kali iwe inapigwa kwa wingi kwa wale jamaa wauza
kanda za wasanii wa Bongo Flava.
Nakumbuka wakati ule
nilipokuwa naweka 100, 100 za shule ili nipate hela za kwenda kununua album za
akina Jay Moe na Juma Nature. Maisha yanaenda kasi mno leo wakina Ommy Dimpoz
wamegoma kutupa huu uhondo.
Unabaki na mshangao ukijua kuwa wasanii kama Rich Mavoko,Ommy Dimpoz wana miaka zaidi ya mitano kwenye game wakiwa hawana japo album moja kwenye makabati yetu.
Unabaki na mshangao ukijua kuwa wasanii kama Rich Mavoko,Ommy Dimpoz wana miaka zaidi ya mitano kwenye game wakiwa hawana japo album moja kwenye makabati yetu.
Siku hizi wanashindana
kwa video bora na sio album bora tena.
Mambo mengi yalitokea hapa katikati na tukasikia mengi pia yaliyokwamisha maisha yale ya kuvutia kupotea. Wanasema “wadosi” walikuwa wakipata kikubwa huku wasanii wakipata kiduchu na kupelekea kususa kutengeneza album na matokeo yake kuishia kutoka nyimbo,kufanya video kali na kusubiri mikataba ya show kila mtu kasahau kuhusu maisha ya album.
Mambo mengi yalitokea hapa katikati na tukasikia mengi pia yaliyokwamisha maisha yale ya kuvutia kupotea. Wanasema “wadosi” walikuwa wakipata kikubwa huku wasanii wakipata kiduchu na kupelekea kususa kutengeneza album na matokeo yake kuishia kutoka nyimbo,kufanya video kali na kusubiri mikataba ya show kila mtu kasahau kuhusu maisha ya album.
Orodha hii inakuletea
album 10 bora zaidi kwenye Bongo Flava ambazo mpaka leo zimeacha historia:
Historia ya Kweli
Mwanasesere Prince Dully
Sykes kwenye ubora wake. Ilikuwa mwaka 2003 album ile ilifuatana na wimbo mkali
zaidi kutoka kwenye album ile na pengine ni wimbo mkali zaidi kutoka kwa
Mr.Misifa,Ungethubutu kusema nini zaidi kuhusu wimbo wa Salome? Kwenye album
ile ungekutana na simulizi nzuri mno tena zenye ukweli ndani yake.
Tamika msichana
aliyemkimbia na kumuachia watoto, Hajisadi mshkaji wake ambaye alikufa kwenye
meli baada ya kutoswa baharini, Nyambizi jimama lilionyesha mahaba
kwake,Sharifa wimbo uliobeba jina la album maana ile ilikuwa ni historia ya
kweli ya msichana aliyekimbia shule na kuyavagaa maisha ya mtaani kwa pupa na
kuambulia Ukimwi, Julietha aliyekuwa anampenda kwa dhati bila kusikia maneno ya
wanafiki ungepata pia simulizi nzuri ya Kijakazi mtoto wa kizaramo aliyeteka
akili ya Dully vya kutosha.
Miika Mwamba ndiye
producer aliyefanya ngoma nyingi zaidi kwenye album hii. Album zake mbili
zilizofuata Handsome ya mwaka 2004 na Hunifahamu ya 2005 hazikuwa na ubora wa
Historia ya kweli.
Ugali
Diamond Jubilee, watu
walikula Ugali jukwaani,moja kati ya show chache zilizoweza kuujaza ule ukumbi.
Toka pale wasanii wengi wamekuwa wakiukimbia ule ukumbi kwa kuogopa kutumbuiza
viti ila Juma Kassim Ally Kiroboto aliweza kufanya maajabu yake kwenye ukumbi
ule.
Akitoka kugombana na mpenzi wake Sinta wakati ule Juma alirudi akiwa na hasira ya mapenzi. Huwezi kubisha album ile ilibebwa na nyimbo nyingi za mapenzi zaidi tofauti kabisa na album yake ya kwanza ya Nini Chanzo iliyotoka mwaka 2001 ukiondoa wimbo wa Sonia, sidhani kama kulikuwa na wimbo mwingine wa mapenzi.
Akitoka kugombana na mpenzi wake Sinta wakati ule Juma alirudi akiwa na hasira ya mapenzi. Huwezi kubisha album ile ilibebwa na nyimbo nyingi za mapenzi zaidi tofauti kabisa na album yake ya kwanza ya Nini Chanzo iliyotoka mwaka 2001 ukiondoa wimbo wa Sonia, sidhani kama kulikuwa na wimbo mwingine wa mapenzi.
Hata album yake
iliyofuata ya Ubinadamu Kazi ya mwaka 2005 haikuwa na nyimbo za mapenzi kama
hii. Sitaki Demu,Ahh Wapi, Inaniuma Sana, Ugali,Rudi Nyumbani, Kisa Demu, Umoja
wa Tanzania, Hali Ngumu – ni nyundo tupu za kwenye album hii ya kiistoria
kwenye Bongo Flava.
Beat nzuri zote kutoka kwa P.Funk toka mwaka 2003 mpaka leo hazijawahi kupoteza ubora wake na huwezi kuwa na hofu ukisema hii ni album bora zaidi kutoka kwa “mhuni” huyu wa Temeke na bora zaidi ya album yake ya kwanza, Nini Chanzo, Zote History ya mwaka 2006 na hata Tugawane Umaskini ya mwaka 2009.
Beat nzuri zote kutoka kwa P.Funk toka mwaka 2003 mpaka leo hazijawahi kupoteza ubora wake na huwezi kuwa na hofu ukisema hii ni album bora zaidi kutoka kwa “mhuni” huyu wa Temeke na bora zaidi ya album yake ya kwanza, Nini Chanzo, Zote History ya mwaka 2006 na hata Tugawane Umaskini ya mwaka 2009.
Kamanda
Daz Baba,Ferooz,
Critic,La Rhumba na Sajo ni muunganiko fulani mtamu wa washkaji kutoka
Azania,Jitegemee na maskani yao kule Kimara.
Walikuwa na umri mdogo mno wakati ule ila nyimbo zao za ujumbe na huzuni zingekuacha ukiwa unawakumbuka muda wote kwa uzito wa mistari yao.
Walikuwa na umri mdogo mno wakati ule ila nyimbo zao za ujumbe na huzuni zingekuacha ukiwa unawakumbuka muda wote kwa uzito wa mistari yao.
Kwa bahati mbaya kwao
haikufata album nyingine yoyote kutoka kwao baada ya album hii ya kihistoria.
Mwisho wa siku Ferooz alikuja na album yake ya Safari huku Daz Baba akija na
Elimu Dunia na wenzao wote walipotea na kundi lao.
Kamanda ni wimbo uliobeba
jina la album na wimbo ulioacha watu wengi midomo wazi kwa majamaa kujichulia
vifo vyao ila Barua ni wimbo uliomaliza kila kitu na kuipeleka album yao sokoni
wakijidai. Nitafanya Nini,Matatizo,Maji ya Shingo Nashuka Rhymes na nyingine
kali zilizoibeba album hii ya kibabe.
Mika Mwamba na P.Funk
Majani ndio wapishi waliotengeneza nyimbo nyingi zaidi kwenye Santuri hii.
Ulimwengu Ndio Mama
More Tech,More Flava,Mo
Skills,Mo Genius, Superman. Maisha ya boarding noma Jay Moe alisema huko ndiko
alipolipata neno Ulimwengu Ndio ,Mama. Hiyo ni mistari fulani mikali kwenye
wimbo huu wa maisha ya boarding kutoka kwenye album ya hii ya kishujaa.
Nyimbo kama Bishoo,Misosi
Mitungi na Pamba, Ni Mshamba,Majukumu, Narudi Shule zilikuwa ni nyimbo kali mno
kutoka kwenye album hii ila wimbo wa “Kama Unataka Demu” unabaki kama wimbo
bora zaidi kutoka kwa Jay Moe.
Kwa wengi Jay Moe
anachukuliwa kama msanii asie na bahati ila niamini mimi na rudi nyuma kidogo
itafute album hii, isikilize kwa utulivu utakuja kugundua madini yalio
mchangani ila watu wameshindwa kustukia. Alikuwa na ushkaji mkubwa mno na
P.Funk na hivyo ni jambo jema ukijua Majani ndio aliyeipika album hii.
AKA Mimi
Albert Mangwea(rip)
kutoka Dodoma na wanae wa East Zoo,Chamber Squad alikuja kuleta kitu bora zaidi
kitakachoishi kwa miaka mingi mno.
Popote unaweza kwenda ila huwezi kukuta album ambayo ndani yake kila wimbo ni hit song. Kwa wasanii wengi unaweza kukuta album ina nyimbo 10 basi nyimbo kali zaweza kuwa 4 au 5 nyingine ni za kujaza album tu iende sokoni ila kwa Ngwea ilikuwa tofauti mno kuanzia wimbo wa kwanza mpaka wa mwisho, zote zilikuwa za moto, nyimbo ambazo zinaishi hata baada ya kutokuwepo kwake.
Popote unaweza kwenda ila huwezi kukuta album ambayo ndani yake kila wimbo ni hit song. Kwa wasanii wengi unaweza kukuta album ina nyimbo 10 basi nyimbo kali zaweza kuwa 4 au 5 nyingine ni za kujaza album tu iende sokoni ila kwa Ngwea ilikuwa tofauti mno kuanzia wimbo wa kwanza mpaka wa mwisho, zote zilikuwa za moto, nyimbo ambazo zinaishi hata baada ya kutokuwepo kwake.
Ghetto Langu ulikuwa
wimbo wa kwanza kwenye album hii. Huu ni ni wimbo uliomtoa Ngwea kutoka msanii
wa kawaida tu mpaka kwenda kuwa staa anayegombaniwa kwenye show.
Mikasi ni wimbo mwingine
mkubwa zaidi uliofuata kwenye album hii huku nyimbo kama Sikiliza, AKA Mimi,
Zawadi,Dakika Moja, Napokea Simu, Bila Muziki,Mademu Zangu,Weekend na She Got A
Gwan zinafuatana kwenye album hii iliyopikwa kiufundi na Majani. Album hii iliyotoka
mwana 2003 ni album kali zaidi ya album yake Nge iliyofuata mwaka 2010.
Funga Kazi
Hii ilikuwa ni album ya
mwisho ya Hard Blastaz Crew kabla ya kila mmoja kwenda na njia yake. Hapo
unawazungumzia Big Willy,Terry Fanani wa kigogo na Profesa Jay.
Likiwa limetoka kubeba
tuzo ya kundi bora la hip hop mwaka 1999 ndio mwaka 2000 walipokuja na album
hii iliyosheeni ngoma kali tu.
Wimbo kama Chemsha Bongo ungekupa ujumbe mzuri mno, ni wimbo uliObadilisha fikra za wazee wengi kuanza kuona kuwa Bongo Flava sio uhuni na ungEpata ujumbe mwanana mno ndani yake.
Wimbo kama Chemsha Bongo ungekupa ujumbe mzuri mno, ni wimbo uliObadilisha fikra za wazee wengi kuanza kuona kuwa Bongo Flava sio uhuni na ungEpata ujumbe mwanana mno ndani yake.
Mamsap ni wimbo mwingine
mkubwa kutoka kwenye album hii, Chuzi Limekubali, Nusu Peponi nusu Kuzimu na
wimbo kama Ehh Mola zingekupa ujumbe mkali mno kama kawaida ya nyimbo za HBC
wakati ule.
Nitakupa Nini
Amiri Jeshi Mkuu wa
Upanga East Coast, Crazy GK, yupo kimya sana siku hizi ila album hii inabaki
kuwa moja kati ya album bora za muda wote kwenye Bongo Flava. Sister Sister ni
wimbo mkubwa mno uliokuwa ukiwaasa vijana na gonjwa hatari la ukimwi. Tutakukumbuka
ni wimbo mwingine uliomuhusu “mshkaji” wake aliyefariki kwa ajali ya gari
pamoja na Kosa Langu,Malaika,Hii Leo,Nitakufaje,Miiko 10 ya Rap, Nitakupa Nini
Mama.
Elimu Dunia
Akiwa kijana mdogo kabisa
tena akiwa ametoka kwenye moja kati ya kundi bora zaidi kwenye Bongo Flava, Daz
Mwalimu alikutana na P.Funk Majani na kutoka pale kila kitu kilibadilika kwenye
maisha yake ya kimuziki. Pengine ni moja kati ya makosa yake makubwa aliyowahi
kuyafanya lakini usingekuwa karibu kuwaza namna hiyo ikiwa nyimbo kama Namba 8,
Wife, Elimu Dunia, Usihukumu zilikuwa na kiwango kikubwa mno na usingeweza
kumlaumu kwa wakati ule.
Namba 8 akiwa na Fid Q
ulikuwa ni wimbo wa taifa na hata ulipotoka Wife na mwana Ngwea nao ukafuata
mkondo huo. Hatujui kwa uwazi nini kilitokea ila baada ya albaum ile kila kitu
kilibadilika na Daz Baba hakuwa kwenye ubora wake tena mpaka leo hii amegeuka
kuwa mwanamuziki wa kawaida pamoja ukubwa wa album hiyo. Mwaka 2004 ndio
ilienda hewani album hii ya kukumbukwa.
Safari
Ferooz na sauti yake ya
kulalamika alikuwa kwenye ubora mkubwa mno kipindi hiki. Ni mmoja kati ya watu
walioibeba Daz Nundaz kwa mabega yao na usingebisha hili ukijua kuwa nyimbo
kama Barua na Kamanda ni nyimbo zilizokuwa na sauti yake zaidi kuliko member
wenzie wa kundi lile.
Alirudi tena akiwa na
peke yake na ngoma yake ya kwanza ya Jirushe akiwa na Jay Moe kutoka pale Bongo
Records kwa P.Funk. Haikuchukua muda akadondosha wimbo bora zaidi katika maisha
yake, Starehe. Hatujakaa vizuri akatuletea Wema Wangu Umeniponza na ngoma nyingine
nyingi kubwa kwenda kukamilisha album hii ilioacha historia kubwa kwenye Bongo
Flava.
Raha Kamili
AY alikuja Dar es Salaam
kama kutoka Morogoro kutafuta maisha akiwa na begi lake tu. Hakuwa na ndugu
wala jamaa wa karibu zaidi ya washkaji zake Buff G na Snare aliosoma nao Ifunda
Sekondari. Yeye, Buff G na Snare walianzisha kundi lao la SOG. Nyimbo za SOG
zililigusa sikio la P-Funk aliyemwalika kwenye studio zake na kutengeneza ngoma
yake iliyompa jina zaidi, Raha tu.
Mwaka 2001, aliachia
album yake Raha Kamili iliyojumuisha nyimbo kama Safi Hiyo, Ni Alfajiri,
Machoni kama watu (ft. Lady JD), Ni raha tu (feat. Complex), Msimamo wako,
Nachotaka uelewe, Mchango wa macho, Raha kamili, Sio kila Siku na zingine.
Machozi, Jasho na Damu
Profesa Jay aka Heavy
weight MC, Wa mitulinga, Mchawi wa Rhymes, Mti Mkavu, ni msanii wa Bongo Flava
mwenye hit songs nyingi zaidi.
Baada ya kuvunjika kwa HBC,Profesa Jay aliamua kuendelea na game na hii ilikuwa album yake ya kwanza akiwa kama msanii huru mwaka 2001. Bongo Dar es Salaam ni wimbo fulani ambao Jay alizungumzia ujanja ujanja wa bongo na kila mtu akiwa tapeli hata muhuri wa ikulu unapata, bila matata na suala la kupewa pesa bandia baada ya kuuza cheni bandia ni kawaida mno ndani ya Bongo. Wimbo kama Niamini alioimba na washkaji zake Terry Fanani na Big Will ulikuwemo kwenye album hii pia.
Baada ya kuvunjika kwa HBC,Profesa Jay aliamua kuendelea na game na hii ilikuwa album yake ya kwanza akiwa kama msanii huru mwaka 2001. Bongo Dar es Salaam ni wimbo fulani ambao Jay alizungumzia ujanja ujanja wa bongo na kila mtu akiwa tapeli hata muhuri wa ikulu unapata, bila matata na suala la kupewa pesa bandia baada ya kuuza cheni bandia ni kawaida mno ndani ya Bongo. Wimbo kama Niamini alioimba na washkaji zake Terry Fanani na Big Will ulikuwemo kwenye album hii pia.
Ndio Mzee, Jina langu,
Piga Makofi na Salamu Babu na Bibi zilikuwa ni nyimbo nyingine zilizoshiba
kwenye album hii ya kibabe.
Nyimbo zingine ni pamoja na Nawakilisha, Yataka Moyo, Piga Makofi na Tathmini.
Nyimbo zingine ni pamoja na Nawakilisha, Yataka Moyo, Piga Makofi na Tathmini.
Fid Q aliwahi kusema
Machozi, Jasho na Damu ni album bora ya karne. “#MachoziJashoNaDamu is an
indisputable/classic/dope/great&prolly the best album of the 1st century,”
aliandika Fid kwenye Twitter.
P.Funk Majani ni producer
aliyefanya ngoma nyingi zaidi kwenye album hii.
Ipi kati ya hizi ni album
bora zaidi kwako?
Tazama video hapa chini..
No comments
+255716829257