Habari mpya

TANZANIA YATUNUKIWA TUZO NA UMOJA WA NCHI ZA AFRIKA..

July 20 2016 Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi, Augustine Mahiga, amezungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo yaliyojadiliwa katika mkutano wa 27 wa Umoja wa nchi za Afrika uliofanyika hivi karibuni Kigali nchini Rwanda.
Waziri mahiga amesema Serikali ya Tanzania imepewa tuzo 2 za masuala ya Ustawi wa Jamii pamoja na ushirikishwaji wa wanawake katika ngazi ya maamuzi ya Serikali na Taasisi mbalimbali katika Mkutano wa 27 wa Umoja  wa Nchi za Afrika (AU) uliofanyika hivi karibuni Kigali nchini Rwanda……..
>>>’Tanzania imetambuliwa na AU kama nchi ambayo kwa miaka 15 sasa  imekua na mikakati mbalimbali  ya kitaifa ya kuzingatia haki za wanawake na kutimiza malengo ya milenia’
Waziri Mahiga aliongeza kuwa Tanzania ni kati ya nchi tano bora katika bara la Afrika ambazo zimepewa tuzo hizo.

No comments

+255716829257