PERUZI HABARI MBALI MBALI ZA ULIMWENGU LEO JULY 8, 2016..

Rais Barack Obama ashutumu
mauaji ya Wamarekani weusi na walipuaji wa kujitoa mhanga washambulia
sehemu takatifu kwa Waislamu wa Kishia nchini Iraq.
1. Obama shutumu mauaji ya weusi Marekani
Gavana wa Minnesota, amesema hadhanii kuwa afisa wa polisi angempiga risasi dereva, ambaye alitolewa kutoka ndani ya gari ambalo mojawepo ya taa yake ya nyumba ilikuwa imevunjika, kama angelikuwa ni mtu mweupe.
Huku hayo yakijiri habari za hivi punde kutoka Marekani, zasema kuwa maafisa wanne wa polisi wamepigwa risasi katika mji wa Dallas nchini humo.
2. Eneo takatifu kwa Washia lashambuliwa Iraq
Bomu moja lililipuka katika lango la kaburi la Sayid Mohammed bin Ali al-Hadi, katika mji wa Balad. Baada ya mlipuko huo, watu kadhaa waliokuwa na silaha, walianza kuwamiminia risasi waumini waliokuwa wakiadhimisha siku kuu ya Eid.
Baadhi ya washambuliaji walijilipua. Zaidi ya watu 30 wamethibitishwa kufariki.
3. Wapakistani 12 wakamatwa Saudi Arabia
Msemaji wa serikali amesema kwamba, mlipuaji wa kujitoa mhanga, alikuwa na umri wa miaka 26 raia wa Saudia, ambaye alikuwa mtumiaji wa dawa za kulevya.
4. Kamanda wa zamani wa jeshi Chile atiwa mbaroni
Idara hiyo ilibuniwa na Jenerali Pinochet na kuwekwa maeneo ya vijijini nchini Chile, ili kuwasaka, kuwakamata na kuwaua wakereketwa wa upinzani.
5. Watu 20 wajeruhiwa kwenye treni Taiwan
Polisi wanashuku kuwa mlipuko huo umetokana na bomu la bomba.
6. Utafiti: Wengi wameridhishwa na Obama
Kati ya mataifa 19 ya waliohojiwa, ni Urusi tu ndilo taifa ambalo lilikuwa na mtazamo hasi, ya urais wa Obama, huku ikiwa tu na asilimia 18 ya wanaopenda utawala wake.
No comments
+255716829257