Myanmar yawaachia wafungwa wote wa kisiasa
Wafungwa wa kisiasa 83 nchini Myanmar wameachiwa huru.
Serikali mpya ya Myanmar ya Bi Aung San Suu Kyi inayongozwa na rais Htin Kyaw imeamuru kuachiwa kwa kundi la pili kubwa la wafungwa wa kisiasa nchini humo.
Kundi la wafungwa wapatao 100 waliachiliwa huru mapema mwezi huu.
Maafisa wamesema hatua hiyo ya kuwaachia wafungwa wa kisiasa ambayo ni miongoni mwa maaamuzi makuu ya kwanza yaliyoanza kutekelezwa na serikali ya Bi San Suu Kyi's, itaendelea
No comments
+255716829257