Habari mpya

Serikali ya Tanzania imeyafutia usajili magazeti 473 leo..

Serikali imefuta usajili wa Magazeti 473 kupitia tangazo lililochapishwa katika gazeti la serikali lenye namba 195 ambapo sababu za kufutwa usajili huo ni kutochapishwa kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.
Magazeti hayo hayataruhusiwa kuchapishwa au kusambazwa kwa njia ya nakala ngumu au kielektroniki na ikiwa mmiliki wa gazeti lililofutiwa usajili angependa kuendelea na biashara milango iko wazi kwa ajili ya kuwasilisha maombi mapya ya usajili kwa kufuata taratibu zilizopo.
Kwa mujibu wa takwimu za ofisi ya msajili wa magazeti, nchi ya Tanzania inayo magazeti na majarida 881 yaliyosajiliwa kisheria.
chanzo: millardayo.com

No comments

+255716829257