Habari mpya

KAA TAYARI ROMA ANAJIKUBALI MWENYEWE MARA TANO..

 
Rapper Roma amesema Tanzania wasanii hawawezi kuwakukubali wenzao kutokana na umimi walio nao ambapo amejita kuwa yeye katika top 5 ya marapper anaowakubali bongo ni yeye mwnyewe ambapo amejitaja maratano.
Hit maker huyo wa mathematics ameyasema hayo katika mahojiano na kipindi cha ladha 3600 cha Efm alipokuwa akitambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la KAA TAYARI akimshirikisha Rapper Darassa na Jose Mtambo.
Amesema wimbo wake wa MECHI ZA UGENINI unamtambulisha vyema akiwa kwenye showz akisisitiza wimbo wake mpya wa KAA TAYARI alioutambulisha leo rasmi katika vyombo vya habari utakua gumzo zaidi.
Aidha Roma amesema hayo kufuatia kauli ya Rapper Wakazi alipotaja top 5 ya Rapperz anaowakubali bila kumtaja Solo Thang jambo lililomfanya Solo kutweet kupitia akaunti yake ya tweeter kuwa Marapper wa Bongo wanaishia kutaja wasanii wanaowakubali wakati bongo flava wanaendelea kufanya biashara.

No comments

+255716829257