Habari mpya

RAPPER JCB ANAAMINI YEYE NI MIONGONI MWA WAASISI NA WALEZI WA MZIKI WA KIZAZI KIPYA BONGO..


Rapper wa Arusha ambaye kwa sasa anaishi Ulaya, JCB amesema haoni tatizo lolote kwa yeye kutosikika kama zamani kwasababu anaamini kile alichokifanya kwenye muziki kinatosha na ni vyema vijana wapya wakapata nafasi.

Akiongea na mtangazaji wa Jembe FM, Jay Jay, rapper huyo alidai kuwa historia itabaki pale pale kuwa yeye ni miongoni mwa rappers waliotengeneza njia kwenye muziki wa Tanzania ambazo sasa zinapitiwa na wasanii wa leo.

Aliongeza kuwa kwa kutambua maisha yana sehemu mbili, aliamua kujiongeza mapema na kufanya mambo mengine ya kumuingizia kipato kuliko kuutegemea muziki.

“Suala la mimi kwamba muziki wangu unashuka kama hivyo hilo sio tatizo. Bado najivunia nitabaki kuwa the best rapper, nimeshachukua tuzo mbili Bongo ambazo wasanii wengi hawajahi hata kupata wakati mpaka sasa wanafanya vizuri. Nshaacha chata naweza kusema,” alisema JCB.

“Kama hip hop ingekuwa demu, nshaitia mimba ina mtoto wangu,” aliongeza.

“Mimi naona sijapotea, nafanya music, na keep it real, narepresent real hip hop".
chanzo: Bongo5

No comments

+255716829257