Habari mpya

PERUZI HABARI KUU ZAIDI ULIMWENGUNI LEO MEI 16..

1. Polisi wasema bomu la Manchester lilikuwa feki

Image copyrightEPAPETER POWELL
Maafisa wa polisi nchini Uingereza wamesema kuwa kifaa kilichopatikana katika uwanja wa Old Trafford, hakikuwa bomu bali lilikuwa kifaa cha mafunzo ya vilipuzi.
Kifaa hicho kiliachwa hapo na kampuni moja ya ulinzi iliyokuwa ikifanya mazoezi na mbwa wa kunusa vilipuzi. Ugunduzi huo ulisababisha mechi ya mwisho ya ligi kuu msimu huu katika uwanja huo wa Manchester United kuahirishwa na mashabiki kuamriwa kuondoka.

2. Rais wa Ufilipino ataka hukumu ya kifo irejeshwe

Image copyrightAFP
Rais mteule wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, amekariri sera zake kali za kukabiliana na uhalifu na ulanguzi wa mihadarati nchini humo.
Amesema kuwa ataagiza maafisa wa ulinzi kuwapiga risasi washukiwa wa ugaidi watakaokaidi amri yao.
Bw Duterte amesema anashinikiza bunge la Congress kurejesha tena adhabu ya kifo.

3. Shirika la Uingereza kusaidia kuondoa mabomu

Image copyrightAFP
Shirika moja la misaada la Uingereza litafanya operesheni ya kuondoa mabomu yaliyotegwa ardhini kuzunguka makanisa saba katika Ukingo wa Magharibu mwa mto Jordan, katika eneo ambalo Wakristo wanaamini kuwa Yesu alibatiziwa.
Eneo hilo lilitekwa na wanajeshi wa Israel mwaka wa 1967, ambao walitega mabomu hayo ya ardhini.

4. Mstari wa wakoloni ulioathiri siasa Mashariki ya Kati

Image copyrightBBC WORLD SERVICE
Mia mia moja iliyopita, watawala wa kikoloni wa Ufaransa na Uingereza walichora mstari mmoja katika ramani ya eneo la Mashariki ya kati, ambayo inaendelea kubadili siasa za kanda hiyo hadi leo.
Mkataba wa kisiri unaojulikana kama Sykes-Picot, ulitenga eneo na ardhi inayoanzia Iran hadi bahari ya Mediterranean, kuwa himaya ya Uingereza na Ufaransa.

5. Waasi wa FARC kuwaachilia watoto

Image copyrightAFP
Serikali ya Colombia imesema imeafikiana mpango wa kuwaachilia watoto wanaotumiwa kwenye vita na kundi la waasi la FARC.
Mkataba huo ulioafikiwa kwenye mazungumzo ya amani mjini Havana, utatoa nafasi kwa wapiganaji walio na chini ya umri wa miaka kumi na mitano waliosajiliwa na kundi hilo la FARC kuachiliwa.
Mkataba huo kisha utawajumuisha wapiganaji wote walio na chini ya umri wa miaka kumi na minane.

6.Waliomuua Mfaransa wafungwa jela Misri

Image copyrightEPA
Na mahakama moja nchini Misri imewahukumu wanaume sita kifungo cha miaka saba gerezani, baada ya kuwapata na hatia ya kumpiga raia mmoja wa ufaransa hadi kufa katika kituo kimoja cha polisi.
Eric Lang, mwenye umri wa miaka 49 na ambaye ni mwalimu alikamatwa miaka mitatu iliyopita mjini Cairo. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, Lang alishambuliwa na wafungwa hao baada ya kuzozana wakiwa kizuizini.

No comments

+255716829257