Habari mpya

Angelique Kidjo apewa tuzo ya haki za kibinaadamu

Image copyright
Image captionAngelique Kidjo
Mwanamuziki wa taifa la Benin aliyeshinda tuzo ya Grammy Angelique Kidjo, pamoja na wanaharakati 3 kutoka barani Afrika wametuzwa tuzo ya haki za kibinaadamu mwaka 2016 kwa kusimamia haki na shirika la Amnesty International.
Kidjo na Enough is Enough (Y'en a marre) wa Senegal, Le Balai Citoyen kutoka Burkina Faso na Lucha kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wameonyesha ujasiri, shirika hilo la haki za kibinaadamu limesema.
Wote wameonyesha kwamba wanapigania haki za kibinaadamu kwa kutumia vipaji vyao kuwashiwishi wengine, Salil Shetty katibu mkuu wa Amnesty International amesema katika taarifa.
Kidjo pia anajulikana kwa kampeni yake kwa uhuru wa kujieleza pamoja na vita dhidi ya ukeketaji.
Mwanamuziki huyo amejiunga na orodha ya watu maarufu ambao wameshinda tuzo ya ubalozi wa watu walio na dhamira ya kubadilisha uovu katika jamii ,akiwemo rais wa kwanza Afrika kusini Nelson Mandela na msanii wa China Ai Weiwei.

No comments

+255716829257