Habari mpya

Waliowabaka wanawake Cologne huenda wasikamatwe



Polisi mjini CologneImage copyrightGetty
Image captionPolisi mjini Cologne wanasema picha CCTV si bora kubaini visa vya ubakaji
Wengi wa wanaume waliowabaka wanawake katika mji wa Cologne wakati wa sherehe za mwaka mpya huenda wasikamatwe, ameeleza mkuu wa polisi mjini humo.
Akizungumza na BBC, afisa huyo, Juergen Mathies amesema kuwa picha za video zilizonaswa na mtambo wa CCTV hazikua nzuri vya kutosha kuwezesha kutambuliwa kwa uhalifu wa kingono.
Maafisa wa usalama wameweza kuwatambua washukiwa 75. Wengi ni kutoka Afrika magharibi walioingia Ujerumani kinyume cha sheria ama kutafuta hifadhi.
Image captionBaadhi ya wakazi wa Cologne wakiwa na mabango ya kupinda mashambulio ya ubakaji mjini Cologne
Zaidi ya malalamiko 500 ya uhalifu yaliwasilishwa kwa polisi, ambapo asilimia 40% yalidaiwa kuwa ni ya ubakaji.
"picha za CCTV si bora kiasi cha kuonyesha wazi vitendo vya ubakaji. Tunaweza kuona baadhi ya vitendo vya wizi, lakini ni hilo tu.
Image captionPolisi wakimpeleka mmoja wa wanaume kutoka eneo la tukio yalikofanyika mashambulio ya ubakaji
''Tunategemea maelezo ya mashahidi na waathiriwa wanaowatambua walio washambulia," alisema Bwana Mathies.
Raia wawili wa Morocco na mtunisia wanatarajiwa kwenda mahakamani baadae kwa tuhuma za wizi, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mtu yeyote kuwahi kupelekwa mahakamani kuhusiana na wizi uliofanyika katika mashambulizi ya mwaka mpya mjini humo.
Wanaume kumi na watatu wamekwisha kamatwa kwa wizi, lakini ni mmoja tu mwenye umri wa miaka 26 raia wa Algerian anaeomba hifadhi ya ukimbizi aliekamatwa kwa akishukiwa kwa ubakaji.

No comments

+255716829257